Skip to main content

Chuja:

wasichana

10 MEI 2023

Jaridani hii leo tunaangazia machafuko nchini Sudan na hali ya wakimbizi wa ndani na wale wanaosaka hifadhi katika nchi jirani. Makala tunaangazia afya ya uzazi na watoto wanaozaliwa njiti  na mashinani tunakupeleka nchini Tanzania, kulikoni?

Sauti
11'30"

27 APRILI 2023

Jaridani leo tunakuletea mada kwa kina ikimulika harakati za kufanikisha kilimo hifadhi nchini Tanzania. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo ripoti ya UNICEFya wasichanan katika ICT, watoto katika mizozo nchini Sudan na chanjo kwa watoto katika ukanda wa Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini. Na katika jifunze Kiswahili hii leo tuko Tanzania kwenye Baraza la Kiswahili la Taifa BAKITA kupata ufafanuzi wa neno"NDUI".

Sauti
12'16"

06 APRILI 2023

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo tunaangazia afya ya uzazi na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya afya ya uzazi salama kwa wanawake kutoka hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando Dk. Elieza Chibwe akizungumzia juu ya kukoma kwa hedhi kwa wanawake anasema “Ukihisi dalili za menopause mapema nenda hospitali.” Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo salamu za sikukuu za Pasaka na Eid El Fitr kutoka kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ombi la UNICEF la msaada kwa watoto waathirika wa matetemeko ya ardhi huko mashariki ya kati, na haki za watu wa jamii asili.

Sauti
13'2"

04 APRILI 2023

Hii leo ni siku ya mada kwa kina ambapo leo tutasafiri pamoja hadi visiwani Zanzibar nchini Tanzania kusikia harakati binafsi za mke wa Rais katika kutekeleza Malengo ya Maendeleo Endelevu ili kusaidia wanawake, wasichana, vijana na watoto. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo za afya uzazi , athari za mabomu ya ardhini na ubaguzi dhidi ya raia weusi nchini Tunisia. Mashinani tunakuletea ujumbe kuhusu athari za mabomu ya ardhini.

Sauti
12'54"

17 MACHI 2023

Hii leo jaridani tunakuletea habari za WHO nchini Burundi na UNICEF eneo la Sahel. Makala tutamsikia mwanafunzi kutoka Tanzania ambaye ni mshiriki wa mkutano wa  67 wa  Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW67 na mashinani tutasalia hapa makao makuu kusikia ujumbe kuhusu haki ya maji.

Sauti
14'5"

16 MACHI 2023

Hii leo jaridani tunanasalia hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa kusikiliza mahojiano yetu na viongozi waandamizi wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto huko Zanzibar Tanzania wanaoshiriki mkutano wa 67 wa hali ya wanawake duniani, CSW67 maudhui yakiwa matumizi ya dijitajitali katika zama za sasa za teknolojia kwa lengo la kusaidia wanawake na wasichana na hatimaye jamii. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo hali nchini Malawi baada ya kimbunga Freddy kuzuka nchini humo, Wakimbizi Ethiopia WHO na teknolojia UNCTAD. Katika kjifunza Klugha ya Kiswahili Dkt.

Sauti
13'23"
UNICEF/Furrer

UN: Wanaume na wavulana jitokezeni mtokomeze FGM

Hii leo ni ikiwa ni siku ya kimataifa ya kutokomeza ukeketaji wa wanawake na wasichana ,Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametaka wanaume na wavulana wapaze sauti zao kusaidia kutokomeza mila hiyo potofu na hatarishi.  

Ujumbe wa siku hii kwa mujibu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa, lile la kuhudumia Watoto, UNICEF na lile la afya ya uzazi na idadi ya watu duniani, UNFPA ni “Nafasi ya ubia na wanaume na wavulana katika kurekebisha maadili ya kijamii na kijinsia ili kutokomeza FGM.”  

Sauti
2'10"
Mtoto akitabasamu darasani wakati wa ziara ya pamoja ya ECW na Norway kwenye maeneo nufaika ya miradi ya elimu inayofadhiliwa na pande mbili hizo.
ECW

Watoto milioni 222 walio katika maeneo yaliyoathirika na migogoro wanahitaji msaada wa haraka wa elimu:ECW 

Mfuko wa Umoja wa Mataifa unaohusika na kusongesha elimu kwenye maeneo yenye majanga na mizozo ya muda mrefu, Education Cannot Wait, ECW au kwa lugha ya Kiswahili, Elimu Haiwezi Kusubiri, pamoja na wadau wamesisitiza umuhimu wa kusaidia mamilioni ya watoto walio katika mazingira ya migogoro ili waweze kupata elimu, wakisema elimu ndio ufunguo wa kuwakomboa watoto hao hususan wasichana katika maisha yao ya siku za usoni.

Sauti
3'7"
UN News Video/Thelma Mwadzaya

Kenya: Mradi wa Teen Seed Africa warejesha matumaini ya elimu kwa wasichana waliopata mimba za utotoni

Umoja wa mataifa kwa ushirikiano na serikali ya Kenya ulizindua mwaka 2015 mradi wa kuwarejesha watoto shule walioacha kwa sababu moja au nyengine. 

Kupitia mashirika mbalimbali kama Educate A Child, Shirika la umoja wa mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na lile la idadi ya watu duniani UNFPA ilizindua miradi ya pamoja ya kuwarejesha watoto shule. 

Utafiti wa hivi karibuni  wa mashirika hayo umebainisha kuwa moja ya chanzo kikuu cha watoto wa kike kuacha shule ni mimba za utotoni na hususan watoto ambao wanaishi katika mitaa ya mabanda.  

Sauti
6'41"

26 JANUARI 2023

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo leo tunakwenda nchini Kenya kuangazia juhudi za mradi wa Teen Seed Africa unavyorejesha matumaini ya elimu kwa wasichana walioacha shule kutokana na mimba za mapema.  Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo kutoka nchini DR Congo, Ethiopia na Senegal. Katika kujifunza Kiswahili   ambapo utapata ufafanusi wa msemo "TABIA NI NGOZI."

Sauti
12'15"