Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ndoto za kuwa daktari au Mwalimu Mkuu kwa watoto hawa zitatimia?

Ndoto za kuwa daktari au Mwalimu Mkuu kwa watoto hawa zitatimia?

Pakua

Ijapokuwa ni wakimbizi wa ndani na wanaishi kwenye kituo cha kuhifadhi wakimbizi wa ndani cha Bushagara, mjini Goma, jimboni Kivu Kaskazini, mtoto Irene anataka kuwa daktari, na Christelle anataka kuwa Mwalimu Mkuu. Ingawa hivyo, elimu bado ni changamoto kubwa kwa watoto milioni 2.4 wakimbizi wa ndani nchini DRC hususan majimbo ya Kivu Kaskazini, Ituri na Kivu Kusini ambao wanahitaji elimu kwa haraka. Hoja ni iwapo ndoto zao hizo zitatimia au ndio zitapeperushwa na vita inayoendelea nchini mwao na kuwafurusha kila uchao? Assumpta Massoi kupitia Makala hii iliyoandaliwa na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya dharura anakuletea simulizi za watoto hao wakiwa Bushagara. 

Audio Credit
Leah Mushi/Assumpta Massoi
Sauti
3'32"
Photo Credit
© UNICEF/Gwenn Dubourthoumieu