Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tumejadili mambo mengi katika Mkutano wa 146 wa Umoja wa Mabunge Duniani - Spika wa Bunge la Tanzania Dkt Tulia Ackson.

Tumejadili mambo mengi katika Mkutano wa 146 wa Umoja wa Mabunge Duniani - Spika wa Bunge la Tanzania Dkt Tulia Ackson.

Pakua

Mkutano wa 146 wa Umoja wa Mabunge Duniani ulioanza tarehe 11 mwezi huu wa Machi na kujumuisha Mabunge ya Nchi Wanachama, Waangalizi wa Kimataifa na Majukwaa mbalimbali ya Kibunge ili kuchagiza Amani na kujenga Jamii Jumuishi na Kuvumiliana umehitimishwa leo tarehe 15 Machi 2023. Katika Mkutano huu Mabunge yameeleza namna ambavyo yameweza kufikia ushirikishwaji wa Vijana, Wanawake na Jamii kwa ujumla katika kulinda amani sambamba na kusisitiza kuheshimu mipaka ya kila mmoja wao. Dhima hii ni msisitizo wa malengo ya Maendeleo Endelevu hususani lengo namba 16 la Umoja wa Mataifa. Zaidi kuhusu yaliyojadiliwa Spika wa Bunge la Tanzania Dkt. Tulia Ackson ambaye ni Rais wa Kundi la Kijiografia na Kisiasa la Mabunge ya Afrika anatueleza yale waliyoyajadili katika Mkutano huo halikadhalika mtazamo wake kuhusu ripoti ya hivi karibuni ya IPU kuhusu idadi ya wabunge wanawake duniani. 

Audio Credit
Flora Nducha/Dkt. Tulia Ackson
Audio Duration
4'20"
Photo Credit
UN NEWS/ Anold Kayanda