10 Novemba 2021
Pakua
Hii leo katika jarida tunakueletea mada kwa kina mahsusi kutoka nchini Tanzania ikiangazia mchango wa vijana na ubunifu wa matumizi ya mifumo ya mawasiliano na teknolojia katika kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs.
Pia utasikia habari kwa ufupi ambao ripoti mbili zimetolewa hii leo na mashirika ya Umoja wa Mataifa moja ikiangazia masuala ya chakula na nyingine ikiangazia watoto wenye ulemavu duniani.
Audio Credit
Assumpta Massoi
Audio Duration
12'20"