Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

27 Mei 2021

27 Mei 2021

Pakua

Hii leo jaridani Leah Mushi anaanzia na habari za ulinzi wa amani ikiwa ni kuelekea siku ya walinda amani duniani tarehe 29 mwezi huu wa Mei. Atakupelekea Ghana kuangazia jinsi ilivyobainika kuwa masomo ya darasani kwa kiasi kikubwa bado hayamwezeshi kijana kujikimu maisha yake mtaani. Huko Ecuador wakimbizi kutoka Colombia wahaha kujikimu na maisha na makala leo tunapiga kambi nchini Kenya kuzungumza na mshindi wa tuzo ya kipekee ya Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya jinsia kwenye ulinzi wa amani. Mashinani tunakwenda Guinea, karibu!

Audio Credit
Leah Mushi
Audio Duration
13'21"