Uvumbuzi wa kifaa kwa ajili ya kukabiliana na nyakati za COVID-19
Na sasa tumwangazie Ombeni Sanga, mvumbuzi kijana mtanzania ambaye ametengeneza kifaa chenye uwezo wa kusambaza elimu katika mazingira ambayo hakuna mwalimu, akilenga zaidi wanafunzi katika kipindi hiki ambapo shule zimefungwa kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa COVID 19.
Ombeni kwa miaka kadhaa amekuwa akijihusisha na ufundi wa vifaa mbalimbali vya kielektroniki kabla ya kupata wazo la kuunda kifaa hiki ambacho anasema kinaweza kuwa na walimu wengi kwa wakati mmoja
Ombeni anasema anaanza kwa kuandaa maandishi kutoka vyanzo mbalimbali kisha anarekodi sauti za walimu wakifundisha mada za msingi za masomo kabla ya kuziingiza sauti hizo katika kifaa chake. Anapata wapi vifaa? Anaeleza?
Kijana huyu mbunifu anasema changamoto aliyonayo kwa sasa ni kuwa ili kuzalisha kwa wingi kifaa hiki kinachotumia betri za kawaida na kisichohitaji intaneti, atalazimika kwenda kiwandani lakini uwezo huo hana kwa sasa. Na sasa kwa mukhtasar hebu tuone kifaa hiki kinavyofanya kazi