Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hatua zaidi zachukuliwa kukabiliana na COVID-19 nchini Kenya

Hatua zaidi zachukuliwa kukabiliana na COVID-19 nchini Kenya

Pakua

Kufuatia raia wa Kenya kulalamikia hatua ya Rais wa nchi hiyo kutangaza zuio la kusafiri katika baadhi ya mikoa kwa mfano kuingia jijini Nairobi, Msemaji wa serikali ya Kenya Cyrus Oguna ameieleza idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa kuwa tangazo hilo la rais Uhuru Kenyatta halina nia ya kumuumiza mtu yeyote bali kuwakinga wananchi wote dhidi ya virusi vya corona, COVID-19. Hadi sasa Kenya imethibitisha kuwa na wagonjwa 172 baada ya watu wengine 14 kugunduliwa kuwa na virusi hatari vya corona kwa muda wa saa 24 zilizopita. Jason Nyakundi ametuandalia makala hii akiwa mjini Nairobi.

Audio Credit
Loise Wairimu/ Jason Nyakundi
Audio Duration
5'26"
Photo Credit
© Julius Mwelu/ UN-Habitat