Majuto mjukuu, kijana tambua ujana ni maji ya moto
Pakua
Nchini Thailand kile kilichoonekana kuwa ni raha ya aina yake kwa msichana mmoja baada ya kukutana na mpenzi wake kupitia mtandao wa kijamii, kimegeuka shubiri baada ya kujikuta na ujauzito bila kujua cha kufanya. Mtoto huyo wa kike aitwaye jina la Fang alikata tamaa ya maisha na kujilaumu kila uchao. Hata hivyo kupitia mradi wa makazi ya dharura unaoungwa mkono na shirika l aUmoja wa Mataifa la idadi ya watu, UNFPA mtoto Fang sasa ameweza kuona nuru kwenye maisha yake. Je nini kimefanyika? Ungana basi na Assumpta Massoi kwenye makala hii.
Audio Credit
Flora Nducha/ Assumpta Massoi
Audio Duration
4'6"