Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, limekaribisha hii leo uamuzi wa serikali ya Thailand ya kuwapa uraia vijana watatu na kocha wao wa soka , ambao hivi karibuni waliokolewa kutoka pangoni huko Chiang Rai katika operesheni isiyo ya kawaida iliyoongozwa na jeshi la nchi hiyo.