Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UN imeazimia kutokomeza kabisa silaha za nyuklia-Guterres

Shirika la kimataifa la nishati ya atomki IAEA imehakiki kuwa vifaa vya nyuklia katika kiwanda cha Dukovany Jamhuri ya Czech ni kwa matumizi ya amani tu.
IAEA
Shirika la kimataifa la nishati ya atomki IAEA imehakiki kuwa vifaa vya nyuklia katika kiwanda cha Dukovany Jamhuri ya Czech ni kwa matumizi ya amani tu.

UN imeazimia kutokomeza kabisa silaha za nyuklia-Guterres

Amani na Usalama

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa  Antonio Guterres amekaribisha maadhimisho ya mwaka mmoja tangu kupitishwa kwa  mkataba  wa kimataifa wa kuzuia silaha za nyuklia, TPNW.

Amesema kupitishwa kwa mkataba huo, Julai 7 mwaka 2017 na mataifa 122, kunadhihirisha uungwaji mkono wa jamii ya kimataifa kuhusu suala liliopo la kukomesha  tishio la silaha za nyuklia.

Ameongeza kuwa hadi sasa mataifa 59 ndio yametia sahihi mkataba huo wa TPNW na mengine 11 yakiwa yameuratibu na endapo mataifa 50 yatauratibu hapo ndipo utaanza  kutekelezwa rasmi, na kuwa chombo muhimu katika kutokomeza silaha hizo.

Katibu Mkuu ,kupitia taarifa iliyotolewa leo mjini New York Marekani na naibu msemaji wake Farhan Haq, amesema kuwa Umoja wa  Mataifa, umeazimia kuondoa kabisa silaha za nyuklia kama será yake ya juu ya unyanganyaji wa silaha hizo.