Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kama walivyo binadamu wanaocheza filamu , wanyama wanastahili kulipwa wanapohusishwa: UNDP

Mbuga la wanyama la kitaifa la Mikumi nchini Tanzania.(Picha ya UM/NICA:149108)

Kama walivyo binadamu wanaocheza filamu , wanyama wanastahili kulipwa wanapohusishwa: UNDP

Masuala ya UM

Wanyama wanahusihwa kwa asilimia 20 kwenye matangazo ya biashara na hata filamu, lakini hawalipwi ujira wowote au kupewa msaada wanaouhitaji, sasa umewadia wakati wa kuwatendea haki.

Kauli hiyo imetolewa na  balozi maalum wa mpango wa kuwasaidia na kuwalinda Wanyama ujulikanao kama  Lions Share , Sir David Attenborough wakati wa uzinduzi wa wakfu maalumu  kwa fuko maalum la ubia kati ya  shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo UNDP, muanzilishi wa wakfu huo FINCH na muanzilishi mwenza MARS kwa lengo la kukabiliana  na changamoto zilizopo  katika uhifadhi wa wanyama pori na  maslahi ya wanyama kwa jumla.  

(SAUTI YA SIR DAVID ATTENBOROUGH)

“Wanyama ni sehemu ya dunia yetu, utamaduni wetu ,  jamii yetu pamoja na lugha zetu na hata pia utengenezaji na usambazaji  wa filamu. Na kwa kweli picha za wanyama huonekana katika matangazo kwa asilimia 20. Licha ya hivyo, kwa kawaida wanyama hawapatiwi msaada wanaouhitaji mpaka sasa.”

Kupitia mfuko huo, washirika watachangia  asilimia 0.5 ya matangazo yake kwa kila tangazo ambalo myama au Wanyama watahusishwa. Pesa hizo zitatumiwa  kusaidia mahitaji ya wanyama na makazi yao duniani kote. MARS ndio mshirika wa kwanza wa matangazo  katika mpango wa Lions Share.

 

Simba anaangalia mazingira yake nchini Kenya.
Photo: UN/DPI Photo
Simba anaangalia mazingira yake nchini Kenya.

Sir David anasema ingawa kiwango hicho ni kidogo lakini haba na haba hujaza kibaba

(SAUTI YA SIR DAVID ATTENBOROUGH)

“ Ingawa asilimia 0.5 inaonekana kama pesa ndogo, lakini endapo watangazaji 10 wakuu duniani wataukubali mpango huu, itamaanisha ni mchango wa kila mwaka wa dola milioni 47.”

Hata hilo lengo lao ni  kiasi gani ?

(SAUTI YA SIR DAVID ATTENBOROUGH)

“ Lengo letu ni kukusanya dola milioni 100 kila mwaka. Kwa kufanya kitu kidogo leo tuna nafasi kubwa ya kubadili mambo kesho.”

Naye mkuu wa  UNDP, Achim Steiner, amesema wanyama pori na makazi yao wako hatarini. Ameongeza kuwa, “tunapoteza aina mbalimbali za wanyama kwa kasi ambayo inakadiriwa kufika mara 1,000 zaidi ya kawaida.” Hivyo mkakati wa  Lion’s share ni wazo zuri ambalo litaleta msukumo kuhusu mustakabali wa wanyama, makazi yao na pia ulimwengu wetu.