Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ban ataka kuwepo Usawa kati ya Kazi na Familia

Ban ataka kuwepo Usawa kati ya Kazi na Familia

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ameelezea umuhimu wa kuwepo usawa kati ya kazi na familia akisema kuwa itakuwa ni manufaa kwa familia na kwa jamii kwa ujumla. Kwenye ujumbe wale wakati wa maadhimisho ya siku ya familia duniani ambayo inaadhimishwa kila terehe 15 mwezi Mei Ban amesema kuwa lengo kuu ni kuzisaidia familia upande kiuchumi na hisia.

Ban amesema kuwa mifumo ya sasa ni bora kwa familia ikiwemo kushiriki kwa wanawake kwenye ajira, kuhamia kwa watu mijini kutafuta ajira pamoja na lizikizo zinazotolewa kazini.