Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNHCR imefichua mapengo kwenye huduma za kimsingi kwa wahamiaji duniani

UNHCR imefichua mapengo kwenye huduma za kimsingi kwa wahamiaji duniani

L. Craig Johnstone, Naibu Kamishna Mkuu wa Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) Alkhamisi aliwasilisha ripoti yenye kuonyesha kuwepo pengo kubwa katika utekelezaji wa ule mradi wa majaribio ya kukidhia mahitaji halisi ya wahamiaji katika mataifa manane yanayohudumiwa na UNHCR – ikijumlisha Cameroon, Ecuador, Georgia, Rwanda, Thailand, Tanzania, Yemen and Zambia.