Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kilimo cha kudumu ndio kinga dhidi ya kutanda kwa majangwa, IFAD imeonya

Kilimo cha kudumu ndio kinga dhidi ya kutanda kwa majangwa, IFAD imeonya

Tarehe 17 Juni huadhimishwa kimataifa kuwa ni Siku ya Kupambana na Ukame na Kutanda kwa Majangwa Duniani. Shirika la UM la Mfuko wa Kimataifa juu ya Maendeleo ya Kilimo (IFAD) limeripoti ya kuwa tatizo la mmomonyoko wa ardhi na kutanda kwa majangwa ni janga lenye kuumiza zaidi kihali wakulima masikini pamoja na wachungaji kwenye maeneo husika. Kwa hivyo IFAD imependekeza hali hiyo irekibishwe, na ilitilia mkazo kwamba tatizo la ukame na kutanda kwa jangwa linaweza kudhibitiwa kwa mfanaikio pindi nchi husika zitakaposhiriki kwenye uekezaji kwenye sekta muhimu ya kilimo, na kwa ushirikiano thabiti na taasisi za kimataifa.~