Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Vikwazo maalumu vyaongezewa muda dhidi ya Cote d'Ivoire

Vikwazo maalumu vyaongezewa muda dhidi ya Cote d'Ivoire

Baraza la Usalama limepitisha kwa kauli moja azimio la kuongeza, kwa mwaka mmoja zaidi, vikwazo vya biashara ya almasi na silaha dhidi ya Cote d’Ivoire. Vile vile azimio limepiga marufuku, na kuwanyima fursa ya kusafiri, baadhi ya raia wazalendo wa Cote d’Ivoire. Baraza lilisitiza ulazima wa makundi yote nchini kuwaruhusu wajumbe wa Kundi la Wataalamu waliopelekwa kuchunguza namna vikwazo vinavyotekelezwa kuenedelza shughuli zao bila pingamizi. Azimio limetaka huduma za Kundi la Wataalamu ziendelezwe nchini kwa mwaka mmoja zaidi.