Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkuu wa UNESCO anashtumu unyanyasaji wa wanahabari Eritrea

Mkuu wa UNESCO anashtumu unyanyasaji wa wanahabari Eritrea

Koichiro Matsuura, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la UM juu ya Ilimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) ameripotiwa akisema ya kwamba hakuridhika hata kidogo juu ya namna waandishi habari wanavyotendewa na wenye madaraka katika Eritrea na vikwazo walioekewa vyombo vya habari dhidi ya uhuru wa kuendeleza kazi zao bila ya kuingiliwa na serekali.