ICTR imetoa hukumu ya kumwachia huru aliyekuwa Waziri wa Elimu Rwanda
Mahakama ya UM juu ya Rwanda wiki hii iliamua, kwa kauli moja, kumwachia huru Andre Rwamakuba, aliyekuwa Waziri wa Elimu wa Rwanda aliyeshtakiwa kushiriki kwenye mauaji ya halaiki katika 1994. Mahakama iliripoti kuwa ilishindwa kupatiwa ushahidi wa kuridhisha ulioweza kuthibitsha kihakika kwamba Rwamakuba ana hatia.