UNEP yasisitiza umuhimu wa kuboresha hewa Afrika kusini ya Sahara
Achim Steiner, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la UM juu ya Hifadhi ya Mazingira (UNEP) katika mkutano wasiku nne uliofanyika mjini Nairobi, Kenya wiki hii kusailia suala la kuboresha hewa katika miji ya Afrika ametilia mkazo umuhimu wa kubuni ushirikiano mpya ili kukabili tatizo hilo kwa mafanikio.