Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Gaza hali ni tete lazima misaada zaidi ipelekwe: WFP

Gaza hali ni tete lazima misaada zaidi ipelekwe: WFP

Pakua

Hali kwa raia walioko Ukanda wa Gaza Mashariki ya Kati inazidi kuwa mbayá kila uchao hasa kutokana na kuendelea kwa operesheni za kijeshi za Israel za agani na ardhini zilizosababisha maelfu ya raia kuendelea kutaabika kwa kukosa mahitaji muhimu ya msingi kama chakula, maji, huduma za afya na mawasiliano limesema shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP. Shirika hili ni ambalo ni moja wa wasambazaji wakubwa wa chakula cha msaada sasa wanahaha kuhakikisha malori zaidi yaliyosheheni chakula na maji yanaingia Gaza kupitia mpaka pekee ulio wazi wa Rafah baina ya Gaza na Misri. Mkurugenzi mtendaji wa shirika hilo amefunga safari hadi Rafah kushuhudia hali halisi. Tuungane na Flora Nducha katika makala hii inayoangazia ziara hiyo.


 

Audio Credit
Anold Kayanda/Flora Nducha
Audio Duration
4'10"
Photo Credit
WFP Video