Malengo yetu yako palepale kukomesha machafuko na ukaliaji wa ardhi ya Palestina: Guterres
"Hadhi ya Jerusalem haiwezi kubadilishwa kwa vitendo vya upande mmoja. Malengo yetu yanabaki palepale kukomesha uvamizi huo na kufikia suluhu ya kuwa na serikali mbili ya Israel na Palestina," huu ni msimamo wa Umoja wa Mataifa, ambao Katibu Mkuu wake amesisitiza leo, akionya dhidi ya kuongezeka kwa mvutano na machafuko, na kusisitiza kujitolea kwake kufanya kazi kwa ajili ya haki ya amani.