Chuja:

Palestine

Shule ambayo watoto wa Kipalestina wanahudhuria huko Jerusalem Mashariki.
Reem Arouri

Malengo yetu yako palepale kukomesha machafuko na ukaliaji wa ardhi ya Palestina: Guterres

"Hadhi ya Jerusalem haiwezi kubadilishwa kwa vitendo vya upande mmoja. Malengo yetu yanabaki palepale kukomesha uvamizi huo na kufikia suluhu ya kuwa na serikali mbili ya Israel na Palestina," huu ni msimamo wa Umoja wa Mataifa, ambao Katibu Mkuu wake amesisitiza leo, akionya dhidi ya kuongezeka kwa mvutano na machafuko, na kusisitiza kujitolea kwake kufanya kazi kwa ajili ya haki ya amani. 

Mkimbizi wa Palestina akiishi kwenye makazi ya UNRWA katika Kambi ya Khan Dunoun, Syria.
UNRWA/Taghrid Mohammad

Palestina inahitaji dola milioni 350 kushughulikia misaada ya kibinadamu: OCHA

Mpango mkakati wa msaada wa kibinadamu HRP wa mwaka 2019 umetoa ombi la dola milioni 350  ili kutoa huduma za msingi kama chakula, ulinzi, huduma za afya, malazi, maji na usafi kwa Wapalestina milioni 1.4 ambao wamebainika kuwa na mahitaji makubwa ya kibinadamu kwenye Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Maghariki likiwemo eneo la Jerusalem Mashariki.

Azimio dhidi ya Marekani lapita, yenyewe yasema halina maana

Ukumbi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa leo Alhamisi uligubikwa na maneno ya vijembe wakati wawakilishi wa nchi 193 wanachama wa Umoja huo walipokuwa wanatoa maoni yao kabla ya kupiga kura ya kutaka Marekani ibadili uamuzi wake wa kutambua Yerusalem kama mji mkuu wa Israel. Flora Nducha na ripoti kamili.

(Taarifa ya Flora Nducha)

Je Yerusalem utakuwa au ni mji mkuu wa Israel?

Ni sakata lililotawala baraza kuu la umoja wa Mataifa hii leo katuika kikao cha dharura mjini New york Marekani.

Kila mwamba ngozi akivutia kwake..

Dkt. Salim azungumzia hatma ya Mashariki ya Kati

Kufuatia mjadala unaoendelea kuhusu hatma ya mji wa Yerusalem huko Mashariki ya Kati na mustakhbali wa suluhu ya mataifa mawili ya Palestin na Israel kwenye ukanda huo, mwanadiplomasia nguli nchini Tanzania Dkt. Salim Ahmed Salim ametaja kile kinachopaswa kuzingatiwa ili amani iwepo.

Dkt. Salim ametoa kauli hiyo wakati akihojiwa na kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa nchini Tanzania, UNIC baada ya mazungumzo yake na wajumbe wa Kamati ya Umoja wa Mataifa kuhusu haki za msingi kwa watu wa Palestina, Dkt. Salim jijini Dar es salaam.