Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Israel

IOM inatoa mahema kote Gaza kwa familia zilizopoteza makazi ili kuwasaidia kukaa salama wakati msimu wa baridi unapokaribia.
© IOM

IOM yapeleka msaada wa makazi kwa Gaza kufuatia mahitaji makubwa baada ya kusitishwa kwa mapigano

Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM) limepeleka zaidi ya vifaa vya misaada 47,000 kwa Gaza tangu kutangazwa kwa usitishaji wa mapigano tarehe 10 Oktoba 2025 ili kusaidia familia zilizofurushwa. Kati ya vifaa hivyo, 31,000 ni vya makazi, ikiwa ni pamoja na mahema 2,500, ili kusaidia watu kujenga tena hisia za usalama na utu wao katikati ya uharibifu mkubwa. Imesema taarifa iliyotolewa leo hii huko Geneva/Amman.

23 OKTOBA 2025

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoangazia siku ya Umoja wa Mataifa na tutasikia kutoka mashinani wananchi na asasi za kiraia zina yapi ya kusema kuhusu shirika hili kubwa na la kipekee linalounganisha nchi wanachama 193 duniani.

Sauti
15'53"

14 OKTOBA 2025

Hii leo jaridani tnakuletea mada kwa kina inayoangazia siku ya Mwalimu Nyerere na tunakupeleka nchini Tanzania ambako kunaendelea juhudi za kuimarisha matumimizi ya lugha ya Kiswahili na utangamano katika Jumuiya ya Afrika Mashairki, manufaa ya kiuchumi na kijami na kuenzi mchango wa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Sauti
11'27"
© WHO

Mateka waachiliwa Gaza, misaada yaanza kuingia - UN

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, leo amekaribisha kwa furaha kuachiliwa kwa mateka wote waliokuwa hai kutoka Gaza, huku mashirika ya misaada yakiripoti kwamba usambazaji wa misaada ya kuokoa maisha sasa unafanyika na misaada inaingia kwa kiwango kikubwa katika eneo hilo lililoharibiwa vibaya na vita: Flora Nducha amefuatilia na hii hapa taarifa yake

Sauti
2'56"