Skip to main content

Chuja:

Peru

UNDP Guatemala/Caroline Trutmann

Baada ya hofu kubwa ya soko Peru, IFAD yaleta matumaini makubwa

Miaka miwili iliyopita, wakulima nchini Peru walikuwa na hofu ya kwamba janga la COVID-19 lingalifuta kabisa masoko yao waliyozoea kuuza mazao kama vile kakao na malimao. Walizoea kuuza sokoni lakini COVID-19 ilifuta masoko hayo kutokana na vizuizi vya kutembea.

Hata hivyo Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa maendeleo ya kilimo, IFAD kupitia mradi wa kuchechemua kilimo vijijini baada ya COVID-19 ulileta nuru na sasa wakulima hawaamini kile wakipatacho. Ni kwa vipi basi? Ungana na Assumpta kwenye makala hii iliyoandaliwa na IFAD. 

Sauti
3'9"
Tuzo ya mazingira ya UNEP 2022 yawaenzi warejesha mifumo ya ikolojia
UNEP/Duncan Moore

Tuzo ya mazingira ya UNEP 2022 yawaenzi warejesha mifumo ya ikolojia

Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa mazingira UNEP leo limetangaza washindi wa tuzo yake kubwa kabisa ya mazingira Champion of the Earth 2022 ikiwaenzi mhifadhi wa mazingira, mfanyabiashara, mwanauchumi, mwanaharakati wa haki za wanawake, na mwanabiolojia wa wanyamapori kwa hatua zao za kuleta mabadiliko ya kuzuia, kusitisha na kubadili uharibifu wa mfumo ikolojia. 

Nchini Peru wanawake wa jamii ya asili ya Awajun wanapata miti kwenye vitalu ili kurejesha misitu iliyoharibiwa.
IFAD Video

Wanawake wa jamii ya asili Peru wachukua hatua kulinda misitu

Kwa takribani wiki moja sasa tumekuwa tukimulika masuala ya tabianchi  na mazingira kwa kuzingatia kuwa hivi sasa mkutano wa 27 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu mabadiliko ya tabianchi, COP27 unaendelea huko Sharm el-Sheikh nchini Misri na lengo ni kusongesha harakati za kukabiliana na kuhimili mabadiliko ya tabianchi ambayo kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres hali  ya sasa ni ya udharura, hatua lazima zichukuliwe.

15 NOVEMBA 2022

Leo katika Jarida la Habari za Umoja wa Mataifa tunakuletea Habari kwa Ufupi zikimulika idadi ya watu kufikia bilioni 8, Mada kwa Kina tunakupeleka Peru kumulika wanawake wa jamii ya asili na upandaji miti, na Mashinani tunamulika polisi wa Umoja wa Mataifa na ulinzi wa amani.

1. Habari Kwa Ufupi:

Sauti
12'12"
© FAO/Aamir Qureshi

Pamba ni zaidi ya kitambaa cha nguo

Leo ni siku yap amba duniani ikiwa ni maadhimisho ya kwanza kabisa ya siku hiyo kuenzi zao ambalo kitabaa chake kinatengeneza mavazi ya kila siku kwenye mkabati mengi ya nguo ni kitambaa kizuri, rahisi kuvaa, kukitunza na kinadyumu kwa muda mrefu. Lakini kwa mujibu wa Umoija wa Mataifa pamba inawakilisha zaidi ya kitambaa kama inavyofafanua taarifa ya Flora Nducha 

Sauti
2'40"
Katika kituo cha ukusanyaji wa pamba Brazil ambako pamba hutenganishwa na mbegu kabla haijashindiliwa na kuhifadhiwa
FAO/Alberto Conti

Pamba, kitambaa kinachositiri  zaidi ya familia milioni 100 duniani:UN

 Leo ni siku ya pamba duniani ikiwa ni maadhimisho ya kwanza kabisa ya siku hiyo kuenzi zao ambalo kitabaa chake kinatengeneza mavazi ya kila siku yaliyosheheni kwenye mkabati mengi ya nguo na ni kitambaa kizuri, rahisi kuvaa, kukitunza na kinadumu kwa muda mrefu. Lakini kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa thamani ya pamba ni zaidi ya kitambaa kama inavyofafanua taarifa ya Flora Nducha 

Sauti
2'40"
UN Photo/John Isaac

Mkuu wa 5 wa Umoja wa Mataifa Javier Pérez  de Cuéllar amefariki dunia

Katibu Mkuu wa 5 wa Umoja wa Mataifa Javier Pérez  de Cuéllar amefariki dunia. Alikuwa na umri wa miaka 100. Assumpta Massoi na ripoti kamili.

(Taarifa ya Assumpta Massoi)

De Cuéllar raia wa Peru ambaye amefariku dunia Jumatano ya Machi 03, alihudumu mihula miwili kwenye Umoja wa Mataifa kuanzia tarehe  Januari mwaka 1982 hadi tarehe 31 Desemba mwaka 1991.

Kufuatia taarifa za kifo chake, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa taarifa kupitia msemaji wake akieleza masikitiko  yake makubwa kufuatia kifo cha de Cuéllar.

Sauti
2'12"