27 Desemba 2021
Pakua
Hii leo jaridani ni mada kwa kina na leo tunabisha hodi nchini Tanzania kuangazia harakati za Umoja wa Mataifa kupitisha shirika lake la chakula na kilimo, FAO za kusongesha kilimo hifadhi kama njia mojawapo ya kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDG sambamba na kukabiliana na madhara ya tabianchi. Tunapata pia kwa ufupi habari zilizopatiwa kipaumbele siku ya leo bila kusahau mashinani ambapo tunabisha hodi nchini Kenya kwa wazee wa jamii ya kiduruma wakijakuelimisha jinsi wanavyohesabu miezi kwa lugha ya kiduruma badala ya kutumia Januari, Februari na kadhalika. Mwenyeji wako leo ni Assumpta Massoi. Karibu!
Audio Credit
Assumpta Massoi
Sauti
11'35"