Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jarida 08 Septemba 2021

Jarida 08 Septemba 2021

Pakua

Wakati dunia ikiadhimisha siku ya kujua kusoma na kuandika leo Septemba 8 Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO linasema kumekuwa na hatua kubwa katika miongo kadhaa iliyopita takwimu za mwaka 2019 zikionesha kwamba asilimia 86 ya watu kote ulimwenguni wana uwezo wa kusoma na kuandika ikilinganishwa na asilimia 68 mwaka 1979. 

Pia utasikia mengine mengi ikiwemo elimu kwa watoto wakimbizi na msaada wa kisaikolojia kwa watoto walio kwenye mizozo. 

 

Audio Credit
Grace Kaneiya
Audio Duration
13'26"