Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tuzo ya Nobel ya mwaka 2020 yaenda kwa WFP

Tuzo ya Nobel ya mwaka 2020 yaenda kwa WFP

Pakua

Kamati ya tuzo ya amani ya Nobel yenye makao yake nchini Norway leo imelitangaza shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP kuwa ndio mshini wa tuzo ya amani ya Nobel kwa mwaka huuu wa 2020.  Anold Kayanda na taarifa zaidi.

Ikitangaza tuzo hiyo kamati imesema “ni kwa sababu ya mchango mkubwa wa WFP katika kupambana na njaa, kwa mchango wake wa kuleta mazingira ya amani katika maeneo yenye migogoro na kwa kuwa chachu ya juhudi za kuzuia njaa kutumika kama silaha ya vita na migogoro.” 

Kwa upande wake WFP ikishukuru kwa tuzo hiyo kupitia ukurasa wake wa Twitter imesema “Hii ni kutambua kazi kubwa ya wafanyakazi wa WFP ambao wanaweka Maisha yao hatarini kila siku ili kufikisha chakula na msaada kwa zaidi ya watu milioni 100 wenye njaa wakiwemo Watoto, wanawake na wanaume kote duniani.” 

Katibu Mkuu wa UN Antonio Guterres (wa pili kulia) na David Beasley(kulia) Mkurugenzi Mtendaji wa wa shirika la mpango wa chakula la Umoja wa Mataifa, WFP wakigawa chakula kwa wakimbizi wapya kwenye makazi ya Imvepi nchini Uganda.
UN /Mark Garten
Katibu Mkuu wa UN Antonio Guterres (wa pili kulia) na David Beasley(kulia) Mkurugenzi Mtendaji wa wa shirika la mpango wa chakula la Umoja wa Mataifa, WFP wakigawa chakula kwa wakimbizi wapya kwenye makazi ya Imvepi nchini Uganda.

Akiipongeza WFP kwa ushindi huo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema “Nimefurahi kwa uamuzi wa kamati ya tuzo ya amani ya Nobel kulitunukia shirika la Umoja wa Mataifa la WFP tuzo ya amani yam waka huu. WFP ndilo shirika la kwanza duniani kuwa msitari wa mbele kukabiliana na kutokuwa na uhakika wa chakula. Waume na wanawake wa WFP wanawanapitia hatari na safari ndefu kufikisha msaada wa kuokoa Maisha kwa wale walioathirika na migogoro, kwa watu wanaotaabika sababu ya majanga, kwa Watoto na familia wasio na uhakika mlo wao unaofuta unatoka wapi.” 

Assumpta Massoi/UNNewsKiswahili
GUTERRES KWA WFP

Guterres ameongeza kuwa katika dunia iliyosheheni inasikitisha kwamba mamilioni ya watu wanalala njaa na mamilioni wengine wako katika hatihati ya baa la njaa kutokana na janga la corona au COVID-19

Amesema hivi sasa dunia inakabiliwa pia na njaa ya ushirikiano wa kimataifa na WFP inalisha njaa hiyo pia, shirika hilo linafanyakazi kubwa zaidi ya kivuli cha kisiasa katika operesheni za kushughulikia mahitaji ya kibinadamu na shirika hilo linatekeleza majukumu yake kwa kutegemea michango kuytoka nchi wanachama kwa kiasi kikubwa na pia kutoka kwa umma. 

Amesisitiza kwamba mshikamano huo unahitajika sasa kushughulikia sio tu janga la COVID-19 lakini changamoto zingine za kimataifa katika zama hizi. 

Hivyo Guterres amesema, “nampongeza Mkurugenzi Mtendaji wa WFP David Beasley na wafanyakazi wote wa WFP kwa kuendeleza maadili ya Umoja wa Mataifa kila siku na kutimiza matakwa ya sisi watu , wakati shirika hili likiadhimisha miaka 75.” 

Audio Credit
Assumpta Massoi/Anold Kayanda
Audio Duration
3'8"
Photo Credit
© WFP/Marco Frattini