Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Vijana changamoto zisiwakatishe tamaa bali ziwape chachu ya kusonga mbele- Isaya

Vijana changamoto zisiwakatishe tamaa bali ziwape chachu ya kusonga mbele- Isaya

Pakua

Umoja wa Mataifa hivi sasa unataka vijana ndio wawe mstari wa mbele katika kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs. Ndio maana kila uchao kupitia mashirika yake mbalimbali chombo hicho chenye wanachama 193 kinapaza sauti kwa vijana kushiriki na kushirikishwa katika kila utekelezaji wa malengo hayo kuanzia kutokomeza umaskini, kusongesha amani, afya na hata  ubia wa  maendeleo. Tayari vijana wanaitikia wito na miongoni mwao ni Isaya Yunge, kijana mjasiriamali wa teknolojia kutoka Tanzania ambaye ni  mwanzilishi wa kampuni ya Soma App na pia mwanzilishi mwenza wa kampuni ya teknolojia ya Smart Kaya au Nyumba Janja. Kampuni zao zimesonga na kubadili maisha ya wengi ikiwemo vijana huku akiwaacha watu wengi wakistaajabu na midomo wazi, lakini Assumpta Massoi wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa alitaka kufahamu safari yake ilikuwa 'tamu tu' au iliambatana na shubiri? Na zaidi  ya yote kulikoni yeye anajinasibu kama 'mtu mwenye matumaini asiyetikisika?'.

Audio Credit
Arnold Kayanda/Isaya Yunge/Assumpta Massoi
Audio Duration
4'38"
Photo Credit
Isaya Yunge