Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mipango miji ni hatua ya kwanza katika ujenzi wa miji salama

Mipango miji ni hatua ya kwanza katika ujenzi wa miji salama

Pakua

Lengo namba  9 la malengo ya maendeleo ya endelevu ya Umoja wa Mataifa yanayofikia ukomo 2030, linazungumzia  miundombinu yenye mnepo,  kuwekeza katika  sekta 

ya viwanda endevelu, na kukuza ubunifu. katika sekta hiyo Umoja wa Mataifa unazihimiza serikali na asasi mbalimbali za kiraia kuzingatia ubora wa miundombinu ili  kujenga miji iliyo salama na yenye ustawi bora katika  jamii.

Wito huo umeanza kuitikiwa na serikali mbalimbali, mathalani nchini Uganda , serikali  ya manispa ya Hoima imechukuwa jukumu la kuhakilisha ujenzi wa barabara na miundombinu vinakidhi viwango stahiki kwa manufaa ya taifa na watu wake. Mwandishi wetu  nchini humo John kibego amezungumza na meya wa Hoima ambaye ameweka bayana mikakati madhubuti ya ujenzi wa mji huo kwa kuzingatia taratibu za mipango miji.

Kwa undani zaidi  kuhusu hilo ungana naye.

Audio Credit
Patrick Newman/ John Kibego
Audio Duration
4'5"
Photo Credit
UN Photo/Manuel Elías