Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Baadhi ya watu hunyimwa haki yao ya kumiliki mali

Baadhi ya watu hunyimwa haki yao ya kumiliki mali

Pakua

Katika mwendelezo wa kupitia ibara za tamko la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa ambalo mwaka huu wa 2018 linatimiza miaka 70, leo inamulikwa ibara ya 17 inayozungumzia haki ya mtu kumiliki mali yeye mwenyewe au kwa ushirika na mtu mwingine au wengine. Ibara hii inazingatia ukweli kwamba baadhi ya watu wananyimwa haki hiyo kwa misingi mbalimbali ikiwemo rangi, jinsia, kabila, dini au umri. Katika basi kuangazia utekelezaji wa ibara hiyo tunajikita katika mtu kunyimwa haki hiyo kwa misingi ya kijinsia na kutufafanulia hayo ungana na Siraj Kalyango katika makala hii.

Audio Credit
Anold Kayanda/Siraj Kalyango
Audio Duration
3'17"
Photo Credit
©UNHCR/O. Akindipe