Haki zote za binadamu kwenye ibara 30 za tamko la haki za binadamu haziachanishiki
Ibara ya 30 ya tamko la kimataifa la haki za binadamu linasema vipi? Jebra Kambole wakili kutoka Tanzania anakuelezea kwa muhtasari.
Ibara ya 30 ya tamko la kimataifa la haki za binadamu linasema vipi? Jebra Kambole wakili kutoka Tanzania anakuelezea kwa muhtasari.
Leo tarehe 10 Desemba mwaka 2018 ni kilele cha maadhimisho ya siku ya haki za binadamu duniani ambapo katika mfululizo wa wetu wa kuchambua ibara kwa ibara za tamko la haki za binadamu, tunatamatisha kwa kuangazia ibara ya 30. Ibara hii inaeleza baya kuwa haki zote zilizomo kwenye tamko hilo lililopitishwa tarehe 10 Desemba mwaka 1948 huko Paris, Ufaransa haziachanishiki. Je hii ina maana gani, wakili Jebra Kambole, kutoka Tanzania ambaye pia ni mwanaharakati wa haki za binadamu anafafanua.
Leo ni siku ya haki za binadamu duniani ambapo ni kumbukizi ya miaka 70 tangu kupitishwa kwa tamko hilo tarehe 10 mwezi desemba mwaka 1948 huko Paris Ufaransa.
Miaka 70 iliyopita tamko la haki za binadamu lilipitishwa, ikiwa ni baada ya vita vikuu vya pili vya dunia.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika ujumbe wake anasema kuwa kwa miaka 70, tamko la kimataifa la Haki za Binadamu limekuwa ni mhimili wa kuangaza masuala ya utu, usawa na ustawi na kuleta mwangaza wa matumaini mahala penye giza.
Leo ni siku ya haki za binadamu duniani ambapo ni kumbukizi ya miaka 70 tangu kupitishwa kwa tamko hilo tarehe 10 mwezi desemba mwaka 1948 huko Paris Ufaransa.
Leo ni siku ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa ikiwa ni tarehe ya kukumbuka kupitishwa kwa azimio la haki za binadamu duniani, UDHR ambalo leo linatimiza miaka 70.
Tarehe 10 Desemba 1948, Umoja wa Mataifa uliridhia tamko la haki za binadamu ambalo kwa miaka yote limekuwa muongozo kwa nchi wanachama kote duniani kutunga sheria zinazolenga kumwakikishia haki kila mwanadamu, na kwa hivyo tarehe 10 Desemba mwaka huu wa 2018, dunia inaadhimisha kutimia kwa miaka 70 ya tamko hilo.
Disemba 10, dunia itaadhimisha miaka sabini tangu kuridhiwa kwa tamko la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa. Nyaraka hii imetajwa kuwa ya kipekee kwani imezingatia haki zote na imejumuisha makundi ya watu wote katika jamii ikiwemo makundi ya watu walio wachache.
Katika mwendelezo wa uchambuzi wa ibara kwa ibara za tamko la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa leo tunamulika ibara ya 27 inayosema kuwa kila mtu ana haki ya kushiriki na kunufaika na tamaduni, sanaa na sayansi ya jamii yake. Hii imenyumbuliwa katika pande mbili ambapo ili kuweza kupata ufafanuzi wa kisheria Grace Kaneiya wa Idhaa hii amezungumza na Dkt. Elifuraha Laltaika, mhadhiri wa sheria kutoka Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira nchini Tanzania na anaanza kwa kufafanua yaliyomo.
Wataalamu huru wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa wamesisitiza haja ya kuamsha tena ari ya utekelezaji wa tamko la haki za binadamu lililozinduliwa yapata miaka 70 iliyopita.
Wiki ijayo, dunia itaadhimisha miaka 70 ya tamko la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu. Ingawa historia ya dunia inaonekana kuwasahau wanawake, mtafiti wa masuala ya haki za binadamu Dkt Rebecca Adami katika kitabu chake cha ‘Wanawake na tamko la haki za binadamu’ anasema wanawake walikuwa na mchango mkubwa katika kuliandaa na kulitekeleza tamko hilo.