Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Je Tanzania ya kijani inawezekana? Dk Mwakaluka

Je Tanzania ya kijani inawezekana? Dk Mwakaluka

Pakua

Umoja wa Mataifa na wadau mbalimbali wamekuwa mstari wa mbele katika uhifadhi wa mazingira ili kubabiliana na tatizo la  tabianchi. Kampeni moja wapo katika ulinzi wa mazingira ni uhifadhi wa misitu ya asili na pia upandaji miti ili kufukia lengo la Umoja wa Mataifa la kuongeza misitu yote ya dunia  kwa asilimia  3 ifikapo mwaka 2030.

Tanzania kwa upande wake  imejiwekea mikakati ya maendeleo ya kitaifa  katika uhifadhi wa misitu ya mwaka  2021 ya  kuweza kuongeza ukubwa wa misitu  ya asili kupitia kampendi " panda mti" yenye lengo la kupanda miti milioni 100 kila mwaka.

Mwandishi wetu Patrick Newman alipata fursa ya kuzungumza na Dk Ezekiel Mwakaluka ambaye ni mkurugenzi wa Misitu na nyuki katika wizara ya maliasili na utalii nchini tanzania . Je nini alichozungumza kuhusu utekelezaji wa mikakati ya serikali kuhusu uhifadhi ya misitu Tanzania? Ungana naye katika makala hii.

Audio Credit
Grace Kaneiya/Patrick Newman/ Dr. Ezekiel Mwakaluka
Audio Duration
3'59"
Photo Credit
Misitu kama hii iko hatarini kutoweka kutokana na uvunaji haramu wa magogo. (Picha:UN-REDD Facebook)