Skip to main content

Chuja:

misitu

UNEP/Lisa Murray

Makao Makuu ya UM: Jukwaa la 18 la Umoja wa Mataifa la misitu limeng’oa nanga leo

Jukwaa la 18 la Umoja wa Mataifa la misitu limeanza leo kwenye makao Makuu ya Umoja huo mjini New York Marekani likiwaleta pamoja wadau mbalimbali wakiwemo nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa, mfumo wa Umoja wa Mataifa, mashirika ya kimataifa na kikanda na wadau wa misitu ili kujadili thamani ya rasilimali hiyo muhimu kwa binadamu na mazingira

Kwa mujibu wa shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa FAO misitu ni chanzo kikubwa cha nishati, chakula na malisho, na hutoa riziki kwa mamilioni ya watu, ikiwa ni pamoja na wengi ambao ni maskini zaidi duniani.

Sauti
2'32"

08 MEI 2023

Hii leo jaridani tanaangazia Jukwaa la Umoja wa Mataifa la misitu linaloendelea hapa makao makuu, vita dhidi ya ukimwi Moldova. Makala tunakupeleka nchini Uganda na Mashinani nchini Rwanda, kulikoni?

Sauti
13'32"
Hali ya utulivu ikirejea baada ya mvua kubwa kwenye msitu wa New York
UN Photo/Mark Garten

Jukwaa la 18 la Umoja wa Mataifa la misitu limeng’oa nanga leo makao makuu ya UN

Jukwaa la 18 la Umoja wa Mataifa la misitu limeanza leo kwenye makao Makuu ya Umoja huo mjini New York Marekani likiwaleta pamoja wadau mbalimbali wakiwemo nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa, mfumo wa Umoja wa Mataifa, mashirika ya kimataifa na kikanda na wadau wa misitu ili kujadili thamani ya rasilimali hiyo muhimu kwa binadamu na mazingira.

Sauti
2'32"

21 MACHI 2023

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina nitasalia hapa hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa katika maandalizi ya mkutano wa maji wa mwaka 2023, unaoanza kesho kumsikia Fr. Benedict Ayodi kutoka shirika la kiamatifa la Wakapuchini wa Fraciscan ambao watakuwa na mjadala maalum kuhusu haki ya maji kwa wote katika mkutano huo. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo zikiwemosiku za UN, UNCTAD na Burundi.  Mashinani tunakuletea ujumbe kuhusu misitu.

Sauti
12'48"
IFAD/ Video Capture

Wakazi wa Embu kwa msaada wa IFAD na serikali Kenya wamepanda miti na kulinda mazingira

Kenya ni moja ya nchi zilizoathirika sana na ukame uliosababishwa na mabadiliko ya tabianchi katika Pembe ya Afrika, lakini sasa baadhi ya wakulima wa nchi hiyo kwa msaada wa mfuko wa kimataifa kwa ajili ya maendeleo ya kilimo IFAD wameamua kuchukua hatua kulinda mazingira, maisha yao na kujenga mnepo kwa kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi. Katika kaunti ya Embu wakulima wamepanda msitu mpya ambao unawapa sio tu jukumu jipya la kuulinda lakini pia kuwa chanzo cha kuwapatia kipato.

Sauti
2'58"

22 Novemba 2021

Karibu kusikiliza jarida leo tunajikita katika mada kwa kina kuangazia harakati za kusongesha viwanda vidogo vidogo barani Afrika hususan nchini Tanzania, kwa kuzingatia kuwa mwishoni mwa wiki ilikuwa ni siku ya viwanda barani Afrika.

Pia utapata fursa ya kusikiliza habari kwa ufupi

Sauti
11'41"