Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UN Women yasaidia majaji wanawake Tanzania kuelimisha umma juu ya rushwa ya ngono

UN Women yasaidia majaji wanawake Tanzania kuelimisha umma juu ya rushwa ya ngono

Pakua

Siku hizi majaji, mahakimu, maafisa wa polisi na askari magereza nchini Tanzania wamekuwa wakijitahidi kuelimisha umma juu ya kutokomeza rushwa ya ngono. Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wanawake, UN Women, katika kuchochea elimu hiyo hivi karibuni lilifadhili chama cha majaji wanawake Tanzania, TAWJA kuandaa kitabu kuelimisha umma na mafunzo juu ya rushwa ya ngono. Mafunzo hayo ni pamoja na  yale yaliyofanyika kwa siku mbili huko Arusha na Mwanza. Afisa wa Mawasiliano wa UN Women, Stephanie Raison, alipata fursa ya kuzungumza na washiriki wawili ambao ni Hakimu mfawidhi Mahakama ya Wilaya ya Mbulu, Judith John Kamala na Wakili Modest Akida wa Arusha juu ya kile walichojifunza.