Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Rais wa Baraza Kuu: Redio Miraya ninakutakieni heri ya miaka mingine 18 ya utendaji

Rais wa Baraza Kuu: Redio Miraya ninakutakieni heri ya miaka mingine 18 ya utendaji

Pakua

Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Dennis Francis mwishoni mwa wiki Juni 16 ametumia sehemu ya muda wa ziara yake nchini Sudan Kusini kukitembelea kituo cha redio Miraya kinachoendeshwa chini ya Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo, UNMISS huku mwisho wa mwezi huu wa Juni redio hiyo ikitimiza miaka 18 tangu kuanzishwa kikisalia kuwa chombo muhimu kwa amani na ustawi wa watu wa Sudan Kusini. Pia akiwa kituoni hapo akaitumia nafasi hiyo kuongelea masuala mengine muhimu ya kijamii ikiwemo elimu. Anold Kayanda ameandaa makala hii kutokana na video iliyoratibiwa na UNMISS.

Audio Credit
Flora Nducha/Anold Kayanda
Audio Duration
3'31"
Photo Credit
UNMISS/Isaac Billy