Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kura mbili za turufu zaipinga rasimu ya azimio la Marekani la “umuhimu mkubwa” kusitisha mapigano Gaza

Vassily Nebenzia, Mwakilishi wa Kudumu wa Urusi katika kura za Umoja wa Mataifa dhidi ya rasimu ya azimio wakati wa mkutano kuhusu hali ya Mashariki ya Kati, ikiwa ni pamoja na suala la Palestina.
UN Photo
Vassily Nebenzia, Mwakilishi wa Kudumu wa Urusi katika kura za Umoja wa Mataifa dhidi ya rasimu ya azimio wakati wa mkutano kuhusu hali ya Mashariki ya Kati, ikiwa ni pamoja na suala la Palestina.

Kura mbili za turufu zaipinga rasimu ya azimio la Marekani la “umuhimu mkubwa” kusitisha mapigano Gaza

Amani na Usalama

Katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lililokaa asubuhi hii ya Machi 22 saa za New York Marekani, Urusi na China zimepinga kwa kura ya turufu rasimu ya azimio la Marekani lililotaka "ulazima" kwa usitishaji mapigano haraka na thabiti "kuwalinda raia kutoka pande zote," kuwezesha uwasilishaji wa misaada inayohitajika na kuunga mkono mazungumzo yanayoendelea kati ya Israeli na Hamas.