Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UN yalaani mashambulizi ya kigaidi kwenye mechi ya kriketi Afghanistan

Mchezo wa Kriketi unapendwa sana Afghanistan
Picha ya UNAMA / Jawad Jalali
Mchezo wa Kriketi unapendwa sana Afghanistan

UN yalaani mashambulizi ya kigaidi kwenye mechi ya kriketi Afghanistan

Amani na Usalama

Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa  Umoja wa Mataifa nchini Afghanistan, amelaani mashambulizi ya kigaidi kwenye michezo ya kriketi katika  mji wa Jalalabad hii leo yaliyokatili maisha ya watu 8 na kujehuri 55.

 

Bwana Tadamichi Yamamoto ambaye ni mkuu wa  ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Afghanistan UNAMA, amesema uchunguzi wa kina umebaini kuwa wahusika wa vitendo hivyo vya kigaidi walilipua mabomu 4 yaliopangwa kwa ustadi ili kufanya madhara makubwa kwenye mkusanyiko wa wanainchi waliokuwa wanashuhudia mechi ya kriketi  baina ya timu hasimu ya kwenye uwanja wa nyumbani.


Kwa niaba ya Umoja wa Mataifa , Bwana Tadamichi Yamamoto ametuma salamu za rambirambi kwa wafiwa, huku akiwatakia ahueni majeruhi wote, na kuitaka serikali kufanya uchunguzi ili kubaini wahusika kwani vitendo hivyo ni ukiukwaji mkubwa wa sheria za kibinadamu na Umoja wa Mataifa.


Mkuu huyo ameongeza kuwa wakati huu wa mfungu ni wakati ambapo wananchi wa Afghanistan waanahitaji amani. Hivyo  jamii ya kimataifa kwa ushirikiano na wenyeji wanatakiwa kupinga vitendo hivyo, na kuruhusu mchakato wa amani ya kudumu kwa ajili ya mstakhabali muzuri wa wananchi wa Afghanistan.