Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Raisi wa BK asema madai ya kumzuia mwakilishi wa Israel kuhutubia ni "uongo uliodhamiria mabaya"

Raisi wa BK asema madai ya kumzuia mwakilishi wa Israel kuhutubia ni "uongo uliodhamiria mabaya"

Raisi wa Baraza Kuu la UM, Miguel D’Escoto ameshtumu leo, kwa kupitia msemaji wake, ya kwamba madai yalioenezwa kwenye vyombo vya habari ya kutomruhusu mjumbe wa Israel kuhutubia kwenye Baraza Kuu kuadhimisha miaka 60 ya Azimio la Mwito wa Kimataifa juu ya Haki za Binadamu, ni madai ambayo, na namnukuu hapa, “yaliojaa tetesi za uongo hakika uliodhamiria maovu.”