Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Afrika yahitaji misaada maridhawa kuimarisha kilimo, NKM

Afrika yahitaji misaada maridhawa kuimarisha kilimo, NKM

Kwenye hotuba ya ufunguzi wa Mkutano wa Kimataifa wa Siku Tatu mjini Tokyo kusailia Maendeleo katika Afrika, yaani Mkutano wa TICAD IV, Naibu KM wa UM Asha-Rose Migiro aliwahimiza wahisani wa kimataifa "kuongeza misaada maridhawa" inayohitajika kidharura kuimarisha shughuli za kilimo barani Afrika, hususan katika kipindi ambapo walimwengu wanakabiliwa na bei kubwa ya chakula katika soko la kimataifa, kitendo ambacho, alitilia mkazo NKM, kinahatarisha kuwadidimiza zaidi mamilioni ya watu Afrika kwenye fukuto la umasikini sugu.