Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Alan Doss atilia mkazo ushirikiano wa kikanda kuimarisha usalama Afrika Magharibi

Alan Doss atilia mkazo ushirikiano wa kikanda kuimarisha usalama Afrika Magharibi

Mjumbe Maalumu wa KM kwa Liberia, Alan Doss katika tafrija ilioandaliwa nchini kuheshimu Watumishi wa Ulinzi wa Jumuiya ya Maendeleo ya Uchumi kwa Mataifa ya Afrika Magharibi (ECOWAS) alitilia mkazo umuhimu wa kukuza ushirikiano wao wa kikanda, juhudi ambazo anaamini ndizo zenye uwezo hakika wa kuimarisha usalama wa eneo zima la Afrika Magharibi.