07 Novemba 2023
Pakua
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Umoja wa Mataifa ulikuwa na siku tano za kuadhimisha Umoja wa Mataifa kutimiza miaka 78 tangu kuanzishwa kwake mwaka 1945 huko San Fransisco nchini Marekani. Maadhimisho yalifanyika kuanzia tarehe 23 hadi 27 Oktoba kwenye mji mkuu, Kinshasa. Byobe Malenga, mwandishi wetu katika taifa hilo la Maziwa Makuu ndio alikuwa shuhuda wetu wa nini kilifanyika.
Audio Duration
11'45"