Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

#DRC

Mkuu wa Operesheni za Ulinzi wa Amani za Umoja wa Mataifa, Jean-Pierre Lacroix ziarani nchini DRC
MONUSCO

Heko MONUSCO na FARDC kwa kulinda raia na kupunguza ghasia za makundi yenye silaha: Lacroix

Huko Bunia, jimboni Ituri Mashariki Mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC,  Mkuu wa Operesheni za Ulinzi wa Amani za Umoja wa Mataifa, Jean-Pierre Lacroix, amepongeza juhudi za pamoja za walinda amani wa Mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo MONUSCO na jeshi la serikali ya Congo, FARDC, katika juhudi za kulinda raia na kupunguza ghasia za makundi yenye silaha.

Sauti
2'36"
Mapema mwaka huu familia zilizohamishwa katika kambi ya Bulengo nje kidogo ya Goma zinakabiliwa na hali mbaya ya baadaye na isiyo na uhakika huku mamlaka ya M23 ikiwaagiza kubomoa makazi yao ya muda.
© WFP/Michael Castofas

Mashariki mwa DRC, UNDP yaomba msaada kusaidia wakimbizi wa ndani kujikwamua

Huko jimboni Kivu Kaskazini, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, juhudi za kidiplomasia zinaendelea kumaliza mapigano, huko nalo shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo, UNDP likitoa wito wa msaada kwa watu waliofurushwa makwao kutokana na mashambulizi ya waasi wa M23, msaada ambao utawasaidia kujenga upya maisha yao na njia zao za kujipatia riziki. 

Sauti
1'58"
© UNICEF/UNI786600/Jospin Benekire.

Licha ya ukata UNICEF yajitahidi watoto nchini DRC warejee shuleni

Wakati ghasia zinazoendelea huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC zinaripotiwa kusababisha zaidi ya watoto milioni 1.8 kutokuweko shuleni, shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF nchini humo linajitahidi kwa udi na uvumba kuhakikisha watoto wanapata elimu kwani ni haki yao ya msingi. Je ni kwa vipi? Anold Kayanda anasimulia zaidi.

Sauti
2'9"

15 Aprili 2025

Karibu kusikiliza jarida la Umoja wa Mataifa ambapo hii leo tunamulika Kongamano la Kimataifa la Kiswahili linalofanyika mjini Kampala Uganda likiwaleta pamoja wadau kutoka kila kona ya Afrika na kwingineko kujadili mikakati ya kukuza lugha hiyo adhimu ya Kiswahili. 

Sauti
9'59"
SOFEPADI

Hali ya usalama ikidorora DRC, hofu sasa ni mustakabali wa watetezi wa haki za binadamu

Hali ya kibinadamu ikiendelea kuzorota mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Mtaalamu Maalumu wa Umoja wa Mataifa anayehusika na hali ya watetezi wa haki za binadamu, Mary Lawlor leo ametoa wito wa msaada wa dharura na wa vitendo kwa watetezi wa haki za binadamu katika eneo hilo. Anold Kayanda na taarifa zaidi.

 

(Taarifa ya Anold Kayanda)

Sauti
1'57"