Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Harakati za Uganda kukuza kiswahili, utafiti wafanyika kujua ni nini kikwazo

Harakati za Uganda kukuza kiswahili, utafiti wafanyika kujua ni nini kikwazo

Pakua

Mnamo tarehe 23 mwezi Novemba mwaka jana 2021, Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la elimu, sayansi na utamaduni, UNESCO liliridhia tarehe 7 mwezi Julai kila mwaka kuwa siku ya kimataifa ya Kiswahili. 
 
Hatua hii imezingatia misingi mbalimbali ikiwemo nafasi ya lugha hiyo katika kuleta utangamano katika jamii, kuwa chanzo cha kipato na hata kusongesha amani na usalama. 
 
Uamuzi huo ulipitishwa huku nchi mbalimbali za Afrika zikichukua hatua kuimarisha matumizi ya lugha hiyo ikiwemo nchini Uganda ambako serikali ya Uganda imeimarisha utafiti kote nchini ili kubaini kwa nini lugha ya Kiswahili haikui kama inavyotarajiwa katika nchi hiyo mwanachama mkongwe wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.  
 
Utafiti huo uliotekelezwa kupitia Idara ya lugha ya Chuo Kikuu cha Makerere ulilenga pia kuhamasisha wananchi kuhusu manufaa ya lugha ya Kiswahili na kubaini mikakati ya kukuza lugha hiyo adhimu huku walengwa zaidi wakiwa ni vijana.  
 
Kwa kina kuhusu kinachofanyika ungana na mwandishi John Kibego akizungumza na Dokta Caroline Asiimwe Mhadhiri kwenye Chuo Kikuu cha Makerere, alipokutana naye akifanya utafiti kuhusu lugha hiyo katika jiji la Hoima magharibi mwa Uganda. 

Audio Credit
Anold Kayanda/John Kibego
Audio Duration
4'21"
Photo Credit
John Kibego