24 JULAI 2020
Katika jarida la mada kwa kina hii leo kutoka Umoja wa Mataifa Flora Nducha anakuletea
-Balozi wa kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa Kenedy Gastorn amesema kifo cha aliyekuwa rais mstaafu wa Tanzania Benjamin William Mkapa si pigo kwa Tanzania tu bali kwa Afrika na Jumuiya ya kimataifa kutokana na mchango wake mkubwa katika masuala ya amani
-Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa leo imesema inatiwa wasiwasi na taarifa kwamba serikali ya Zimbabwe huenda inatumia janga la COVID-19 kama chambo cha kubinya uhuru wa kukusanyika na kujumuika
-Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limetoa wito kwa mataifa kuwaachilia wakimbizi na waomba hifadhi walio mahabusu kinyume cha sheria na kuwalinda na janga la COVID-19
-Mada yetu kwa kina leo inamlenga msanii mashuhuri wa uchoraji na uchongaji kutoka Tanzania
-Na katika kujifunza Kiswahili utasikia maana za neno "TRELA" kutoka kwa mchambuzi wetu Onni Sigalla wa BAKITA Tanzania