Wakimbizi si maadui, ni watu wa kawaida waliokimbia kwao kutokana na taabu- Mariella
Shida inapobisha hodi mara nyingi binadamu hukata tamaa na kuamini kuwa huo ndio mwisho wa maisha yake. Ingawa hiyo kwa wengine kukata tamaa ni mwiko kwa kuwa wanaamini kuwa mlango mmoja ukifungwa, mingine mingi hufunguka. Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa Mariela Shaker, mkimbizi kutoka Syria ambaye alipo hii leo, katu hakuna mtu ambaye angaliwaza kuwa angaliweza kufika. Vita, mateso, ghasia, ndio yalikuwa mazoea hadi siku ambayo anakwenda kuchukua diploma yake baada ya kuhitimu chuo, kombora likasambaratisha ndoto zote. Hata hivyo baada ya kuamini kuwa ana fursa nyingine alisaka shule na kukubaliwa chuo kimoja kikuu nchini Marekani. Hii leo ni mtumbuizaji wa kutumia fidla huku akitoa simulizi za alikotoka na kutia moyo watu kupitia shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR. Kwa kina basi Flora Nducha anakusimulia.