Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Narudi nyumbani nikiwa askari bora zaidi- Ngondi

Narudi nyumbani nikiwa askari bora zaidi- Ngondi

Pakua

Meja Jenerali Leonard Ngondi amemaliza muda wake kama mkuu wa vikosi vya Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Liberia UNMIL.

Katika mahojiano na idhaa hii, amesema kwamba amejifunza mengi na anarejea nyumbani Kenya akiwa askari bora kuliko alivyokuwa wakati alipochukua nafasi hiyo takriban miaka miwili iliyopita.

Baada ya kuwasilisha ripoti yake hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa, Meja Jenerali Ngondi  amezungumza na Grace Kaneiya, na hapa anaanza kwa kutaja mafanikio yake makubwa wakati akishikilia nafasi ya mkuu wa vikosi vya UNMIL.

Photo Credit
Meja Jenerali Ngondi (kushoto). Picha: UNMIL