Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

India: Majiko yaliyoboreshwa yaondolea adha wanawake kuvaa miwani wakipika

India: Majiko yaliyoboreshwa yaondolea adha wanawake kuvaa miwani wakipika

Pakua

Katikati ya bonde la mto Ganges kaskazini mwa India, ndiko liko jimbo la Bihar ambalo sasa linahaha kutokana na uchafuzi wa hewa, kwani moshi utokao kwenye majiko ya kuni na samadi ya ng’ombe yanasababisha kwa kiasi kikubwa uchafuzi wa hewa. Licha ya maendeleo makubwa ya kutumia gesi kama chanzo cha nishati, halikadhalika nishati itokanayo na samadi, bado familia au kaya maskini zinashindwa kumudu vyanzo hivyo na kujikuta vikutumia kuni au samadi ya ng’ombe kupikia, ambavyo huchafua hewa. Sasa Benki ya Dunia imewezesha kuundwa kwa vikundi vya kujiwezesha au SHGs ambapo wanawake wanapatiwa elimu ya masuala mbali mbali ikiwemo nishati salama na hivyo kuboresha afya zao. Assumpta Massoi kupitia video ya Benki ya Dunia amefuatilia mradi huo na kuandaa makala hii. 

Audio Credit
Anold Kayanda/Assumpta Massoi
Sauti
2'44"
Photo Credit
Benki ya Dunia