Digrii zangu mbili nimeziingiza katika uuzaji makande na ninafaidika sana- Nancy Lema
Tatizo la ajira kwa vijana nchini Tanzania limeendelea kuwa changamoto kwa vijana wengi, baadhi uhitimu elimu ya juu na vyuo vya kati huku wakiingia mtaani na kuisaka ajira kwa muda mrefu bila mafanikio. Kwa mujibu wa ripoti ya juu ya takwimu za utafiti wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi uliofanywa na Shirika la Takwimu nchini Tanzania (NBS) mwaka 2014, kuwa watu elfu 23, sawa na asilimia 10 ya nguvu kazi, hawana kazi. Nancy Lema ni mtanzania na mhitimu wa shahada ya uzamili kutoka Chuo Kikuu cha mtakatifu Maria kilichopo Minesota nchini Marekani katika fani ya usimamizi wa miradi yaani Project Management ambaye aliporejea nchini Tanzania alikaa miaka mitatu akisaka ajira na ndipo akapata wazo la kuanzisha biashara yake mwenyewe. Evarist Mapesa wa redio washirika SAUT FM ya Mwanza Tanzania, anasimulia zaidi.