Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Natamani mwanangu arejee hali ya kawaida na atembee- Niveen

Natamani mwanangu arejee hali ya kawaida na atembee- Niveen

Pakua
Mgonjwa wa kwanza wa polio kubainika Gaza huko Mashariki ya Kati baada ya miaka 25 ni mtoto wa kiume mwenye umri wa miezi 10. Mtoto huyo na mama yake pamoja na familia nzima wamekuwa wakihamahama na hivyo akakosa chanjo dhidi ya polio. Amri za Israeli za kutaka wapalestina wahame mara kwa mara sasa zinaleta madhara kwa asilimia 90 ya wakazi wa Gaza. Mashirika ya Umoja wa Mataifa likiwemo la Afya, WHO, la kuhudumia watoto, UNICEF na la kuhudumia wakimbizi wa kipalestina, UNRWA wamejipanga kupatia chanjo watoto 640,000 huko Gaza wiki chache zijazo. Lakini mipango hiyo ikiendelea, Assumpta Massoi kupitia mahojiano yaliyofanywa na Ziad Tarib wa Idhaa ya Umoja wa Mataifa huko Ukanda wa Gaza, anakuletea makala inayojikita kwenye simulizi ya mama wa mtoto aliyepooza, changamoto na ndoto zake.


 

Audio Credit
Cecily Kariuki/Assumpta Massoi
Audio Duration
3'51"
Photo Credit
UN News/Ziad Taleb