Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Waathirika Garisa Kenya washukuru UNICEF kwa msaada wa fedha baada ya mafuriko

Waathirika Garisa Kenya washukuru UNICEF kwa msaada wa fedha baada ya mafuriko

Pakua

Kenya inashuhudia kiwango kikubwa cha mvua zaidi ya kile cha kawaida ambacho kimesababisha mafuriko makubwa,maporomoko ya udongo na maelfu ya watu kutawanywa hivi karibuni. Miongoni mwa maeneo yaliyoathirika zaidi ni Kaunti ya Garisa , ambako hivi sasa asante kwa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na wadau wake kama shirika la Norway kwa ajili ya ushirikiano wa maendeleo NORAD, Mamlaka ya Kitaifa ya kudhibiti Ukame Kenya NDMA, na serikali ya Kaunti ya Garasa  kwani kaya zilizoathirika na mafuriko zinapokea msaada wa fedha taslim kupitia M-pesa na vocha za kielektroniki ili kujikimu kimaisha. Flora Nducha anafafanua zaidi katika makala hii

Audio Credit
Leah Mushi/Flora Nducha
Sauti
3'11"
Photo Credit
UNICEF