Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Angola: Mradi wa IFAD umeniheshimisha Kijiji kwetu- Albertina

Angola: Mradi wa IFAD umeniheshimisha Kijiji kwetu- Albertina

Pakua

Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Kilimo, IFAD ni taasisi ya fedha ya kimataifa na pia shirika la Umoja wa Maitafa lililojikita katika kutokomeza umaskini na njaa kwenye maeneo ya vijijini yaliyoko katika nchi zinazoendelea. Miongoni mwa maeneo ambako Mfuko huo unafanya kazi ni nchini Angola barani Afrika ambako huko takwimu zinaonesha ongezeko la vijana wanaohamia mijini kutoka vijijini kwa sababu ya umaskini wa vijijini. Kwa kutambua hilo, na kwa kusaka kuchagiza ufanikishaji wa lengo namba 1 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs kuhusu kutokomeza umaskini, Mfuko huo ukachukua hatua ya kuanzisha mradi wa kuepusha vijana kukimbilia mijini kwani vijijini nao kuna fursa. Ili kufahamu mradi huo ulioleta matokeo chanya, ungana na Assumpta Massoi kwenye makala hii iliyofanikishwa na IFAD.

Audio Credit
Flora Nducha/Assumpta Massoi
Sauti
4'36"
Photo Credit
© FAO/IFAD/WFP/Eduardo Sotera