Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Michezo ni daraja hata katika vita dhidi ya utumikishaji watoto

Michezo ni daraja hata katika vita dhidi ya utumikishaji watoto

Pakua

Katika kampeni ya kupiga vita utumikishwaji  wa watoto  kama askari katika maeneo ya migogoro ya vita inayoendeshwa na  shirika la Umoja wa Mataifa  la kuhudumia watoto UNCEF, imeamua kugeukia michezo kufikisha ujumbe kutokana na uwezo wa michezokuunganisha watu.Uwakilishi wa Ujerumani kwenye Umoja wa Mataifa ukaongeza nguvu katika kampeni hiyo kwa kuwaalika magwiji wastaafu wa kandanda waliowahi kuichezea ligi ya soka ya Ujerumani au  Bundesliga  kuja Umoja wa Mataifa kushiriki mechi kwa lengo la kuchagiza vijana na mashabiki wengine kuhusu kampeni hiyo.

Ujumbe  uliobebwa na kampeni hiyo ni “nguvu ya michezo katika kuwaunganisha watu  kuelekea kwenye kombe la Dunia litakalofanyika nchini Urusi.” Kombe hilo ambalo ni moja ya  mikusanyiko mikubwa kabisa duniani inayowaleta pamoja mamilioni .

Mwandishi wetu Patrick Newman alipata fursa ya kufuatilia hafla ya kampeni  hiyo ya kihistoria iliyoambatana na kabumbu kwa katika viwanja vya Umoja wa Mataifa . Ungana naye katika makala hii upate undani zaid

Audio Duration
4'40"
Photo Credit
Picha ya UN